Tuesday 9 July 2013

MBUNGE WA DODOMA MJINI DAVID MALLOLE AWATEMBELEA WAHANGA WAMLIPUKO WA PETROL HOSPITAL YA MKOA WA DODOMA



Mbunge wa Dodoma mjini  Mh Dr David Mallole, alipoenda kuwatembelea wahanga wa mlipuko wa Petrol katika hospital ya mkoa wa Dodoma,General Hospital na kutoa pole kwa wagonjwa waliopatwa na janga hilo kwa kuwapatia pole pamoja na msaada wa pesa ya dawa kwa kila mmoja , tukio hilo lilitokea juzi saa 12.30 jioni katika Kitongoji cha Machaka, Kata ya Nzughuni.
 Katika tukio hilo marehemu alinunua mafuta ya petroli lita tano katika kituo cha mafuta cha Nanenane na kisha kujilipua.

“Juma ambaye ni mwanafunzi wa fani ya ufundi wa magari, alimwaga petroli hiyo ndani ya saluni ya Irene Mapunda na kujilipua. :Mh baada ya kuguswa na tukio hilo na kuwapa pole :

Maskini mtoto huyu ni mwanafunzi wa kidato cha tatu Shabani p. Shaban naye alikutana na janga hili baada ya kwenda kwa fundi kuchukua nguo zake za shule ambapo ni eneo jirani na mlipuko huo ulipotokea, pia Mh Mbunge David Mallole ameahidi kumlipia ada yake ya shule:








No comments:

Post a Comment