Friday 6 September 2013

RAISI KIKWETE NA KAGAME WAMALIZA TOFAUTI ZAO NA KUKUBALIANA KUSHIRIKIANA KAMA ZAMANI



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete leo, Alhamisi, Septemba 5, 2013, amekutana kwa faragha na Rais wa Rwanda, Mheshimiwa Paul Kagame katika mazungumzo yaliyokwenda vizuri na kuwaridhisha viongozi hao wawili wa nchi jirani. 

Viongozi hao wamekutana kwa zaidi kidogo ya saa moja katika mkutano uliofanyika kwenye Hoteli ya Munyonyo Commonwealth Resort, nje kidogo ya mji wa Kampala, Uganda. 

Katika mazungumzo hayo, Rais Kikwete na Rais Kagame wamekubaliana kuendelea kushirikiana katika kujenga uhusiano mzuri na wa kihistoria uliopo kati ya nchi hizo mbili

Viongozi hao wawili wako nchini Uganda kuhudhuria Mkutano wa Nchi Wanachama wa Umoja wa Kimataifa wa Maziwa Makuu – “International Conference on the Great Lakes Region (ICGLR)” unaofanyika leo Hoteli ya Munyonyo Commonwealth Resort. 

Viongozi wengine ambao wanahudhuria Mkutano huo ni pamoja na Rais Yoweri Museveni wa Uganda ambaye ni Mwenyekiti wa ICGLR na mwenyeji wa Mkutano huo, Rais Silva Kiir wa Sudan Kusini, Rais Joseph Kabila wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika (AU). 

Rais Kikwete na ujumbe wake amewasili Kampala asubuhi ya leo akitokea mjini Dodoma ambako aliwasili jana jioni kwa ajili ya hafla ya kuwaapisha Makatibu Wakuu watatu na Naibu Makatibu Wakuuu wawili iliyofanyika Ikulu Ndogo, Dodoma. 
 
Rais Kikwete aliwasili Dodoma akitokea Mwanza ambako alihudhuria mazishi ya Kiongozi Mkuu wa Kanisa la Evangelistic Assemblies of God Tanzania (EAGT) Askofu Mkuu Dkt. Moses Samwel Kulola yaliyofanyika kwenye Kanisa la Bugando Calvary Temple, mjini Mwanza. 
 
Imetolewa na;
 Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, 
Ikulu, 
DAR ES SALAAM. 
 05 Septemba, 2013 
---------------------
 
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Rais Paul Kagame wa Rwanda wakati walipokutana faragha sambamba na mkutano wa wakuu wa nchi za Maziwa Makuu uliofanyika katika Hoteli ya Munyonyo Commonwealth Resort, jijini Kampala,Uganda, leo
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete, akiwa katika mazungumzo na Marais Paul Kagame wa Rwanda(kushoto), Rais Salva Kiir wa Sudan ya kusini na Rais Yoweri Kaguta Museveni wa Uganda 
Baadhi ya viongozi wan chi za jumuiya ya Maziwa Makuu wakiwa katika picha ya pamoja wakati wa Mkutano wa wakuu wa nchi hizo uliofanyika jijini Kampala Uganda leo.Kutoka kushoto ni Rais Salva Kiir wa Sudani ya Kusini,Rais Joseph Kabila wa DRC,Rais Dkt.Jakaya Kikwete,Rais Yoweri Museveni wa Uganda,Mwenyekiti wa kamisheni ya Umoja wa Afrika Dkt.Nkosazana Dlamini Zuma na Rais Paul Kagame wa Rwanda.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika mazungumzo na Rais Paul Kagame wa Rwanda wakati walipokutana na kufanya mazungumzo ya faragha, katika Hoteli ya Munyonyo Commonwealth Resort, jijini Kampala

RAISI KIKWETE NA KAGAME WAMALIZA TOFAUTI ZAO NA KUKUBALIANA KUSHIRIKIANA KAMA ZAMANI



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete leo, Alhamisi, Septemba 5, 2013, amekutana kwa faragha na Rais wa Rwanda, Mheshimiwa Paul Kagame katika mazungumzo yaliyokwenda vizuri na kuwaridhisha viongozi hao wawili wa nchi jirani. 

Viongozi hao wamekutana kwa zaidi kidogo ya saa moja katika mkutano uliofanyika kwenye Hoteli ya Munyonyo Commonwealth Resort, nje kidogo ya mji wa Kampala, Uganda. 

Katika mazungumzo hayo, Rais Kikwete na Rais Kagame wamekubaliana kuendelea kushirikiana katika kujenga uhusiano mzuri na wa kihistoria uliopo kati ya nchi hizo mbili

Viongozi hao wawili wako nchini Uganda kuhudhuria Mkutano wa Nchi Wanachama wa Umoja wa Kimataifa wa Maziwa Makuu – “International Conference on the Great Lakes Region (ICGLR)” unaofanyika leo Hoteli ya Munyonyo Commonwealth Resort. 

Viongozi wengine ambao wanahudhuria Mkutano huo ni pamoja na Rais Yoweri Museveni wa Uganda ambaye ni Mwenyekiti wa ICGLR na mwenyeji wa Mkutano huo, Rais Silva Kiir wa Sudan Kusini, Rais Joseph Kabila wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika (AU). 

Rais Kikwete na ujumbe wake amewasili Kampala asubuhi ya leo akitokea mjini Dodoma ambako aliwasili jana jioni kwa ajili ya hafla ya kuwaapisha Makatibu Wakuu watatu na Naibu Makatibu Wakuuu wawili iliyofanyika Ikulu Ndogo, Dodoma. 
 
Rais Kikwete aliwasili Dodoma akitokea Mwanza ambako alihudhuria mazishi ya Kiongozi Mkuu wa Kanisa la Evangelistic Assemblies of God Tanzania (EAGT) Askofu Mkuu Dkt. Moses Samwel Kulola yaliyofanyika kwenye Kanisa la Bugando Calvary Temple, mjini Mwanza. 
 
Imetolewa na;
 Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, 
Ikulu, 
DAR ES SALAAM. 
 05 Septemba, 2013 
---------------------
 
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Rais Paul Kagame wa Rwanda wakati walipokutana faragha sambamba na mkutano wa wakuu wa nchi za Maziwa Makuu uliofanyika katika Hoteli ya Munyonyo Commonwealth Resort, jijini Kampala,Uganda, leo
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete, akiwa katika mazungumzo na Marais Paul Kagame wa Rwanda(kushoto), Rais Salva Kiir wa Sudan ya kusini na Rais Yoweri Kaguta Museveni wa Uganda 
Baadhi ya viongozi wan chi za jumuiya ya Maziwa Makuu wakiwa katika picha ya pamoja wakati wa Mkutano wa wakuu wa nchi hizo uliofanyika jijini Kampala Uganda leo.Kutoka kushoto ni Rais Salva Kiir wa Sudani ya Kusini,Rais Joseph Kabila wa DRC,Rais Dkt.Jakaya Kikwete,Rais Yoweri Museveni wa Uganda,Mwenyekiti wa kamisheni ya Umoja wa Afrika Dkt.Nkosazana Dlamini Zuma na Rais Paul Kagame wa Rwanda.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika mazungumzo na Rais Paul Kagame wa Rwanda wakati walipokutana na kufanya mazungumzo ya faragha, katika Hoteli ya Munyonyo Commonwealth Resort, jijini Kampala

RAISI KIKWETE NA KAGAME WAMALIZA TOFAUTI ZAO NA KUKUBALIANA KUSHIRIKIANA KAMA ZAMANI



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete leo, Alhamisi, Septemba 5, 2013, amekutana kwa faragha na Rais wa Rwanda, Mheshimiwa Paul Kagame katika mazungumzo yaliyokwenda vizuri na kuwaridhisha viongozi hao wawili wa nchi jirani. 

Viongozi hao wamekutana kwa zaidi kidogo ya saa moja katika mkutano uliofanyika kwenye Hoteli ya Munyonyo Commonwealth Resort, nje kidogo ya mji wa Kampala, Uganda. 

Katika mazungumzo hayo, Rais Kikwete na Rais Kagame wamekubaliana kuendelea kushirikiana katika kujenga uhusiano mzuri na wa kihistoria uliopo kati ya nchi hizo mbili

Viongozi hao wawili wako nchini Uganda kuhudhuria Mkutano wa Nchi Wanachama wa Umoja wa Kimataifa wa Maziwa Makuu – “International Conference on the Great Lakes Region (ICGLR)” unaofanyika leo Hoteli ya Munyonyo Commonwealth Resort. 

Viongozi wengine ambao wanahudhuria Mkutano huo ni pamoja na Rais Yoweri Museveni wa Uganda ambaye ni Mwenyekiti wa ICGLR na mwenyeji wa Mkutano huo, Rais Silva Kiir wa Sudan Kusini, Rais Joseph Kabila wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika (AU). 

Rais Kikwete na ujumbe wake amewasili Kampala asubuhi ya leo akitokea mjini Dodoma ambako aliwasili jana jioni kwa ajili ya hafla ya kuwaapisha Makatibu Wakuu watatu na Naibu Makatibu Wakuuu wawili iliyofanyika Ikulu Ndogo, Dodoma. 
 
Rais Kikwete aliwasili Dodoma akitokea Mwanza ambako alihudhuria mazishi ya Kiongozi Mkuu wa Kanisa la Evangelistic Assemblies of God Tanzania (EAGT) Askofu Mkuu Dkt. Moses Samwel Kulola yaliyofanyika kwenye Kanisa la Bugando Calvary Temple, mjini Mwanza. 
 
Imetolewa na;
 Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, 
Ikulu, 
DAR ES SALAAM. 
 05 Septemba, 2013 
---------------------
 
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Rais Paul Kagame wa Rwanda wakati walipokutana faragha sambamba na mkutano wa wakuu wa nchi za Maziwa Makuu uliofanyika katika Hoteli ya Munyonyo Commonwealth Resort, jijini Kampala,Uganda, leo
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete, akiwa katika mazungumzo na Marais Paul Kagame wa Rwanda(kushoto), Rais Salva Kiir wa Sudan ya kusini na Rais Yoweri Kaguta Museveni wa Uganda 
Baadhi ya viongozi wan chi za jumuiya ya Maziwa Makuu wakiwa katika picha ya pamoja wakati wa Mkutano wa wakuu wa nchi hizo uliofanyika jijini Kampala Uganda leo.Kutoka kushoto ni Rais Salva Kiir wa Sudani ya Kusini,Rais Joseph Kabila wa DRC,Rais Dkt.Jakaya Kikwete,Rais Yoweri Museveni wa Uganda,Mwenyekiti wa kamisheni ya Umoja wa Afrika Dkt.Nkosazana Dlamini Zuma na Rais Paul Kagame wa Rwanda.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika mazungumzo na Rais Paul Kagame wa Rwanda wakati walipokutana na kufanya mazungumzo ya faragha, katika Hoteli ya Munyonyo Commonwealth Resort, jijini Kampala

RIPOTI MAALUMU KUHUSU VURUGU ZILIZOTOKEA JANA BUNGENI.

 

Jana, Bingwa wa Dunia wa uzani wa kati (super middle), unaotambuliwa na Shirikisho la Ngumi Duniani (WBF), Francis Cheka alitembelea Bunge baada ya kutwaa taji hilo karibuni na jana hiyohiyo, Bunge hilo lilishuhudia ngumi kavukavu katika vurugu kubwa pengine kuliko zote zilizowahi kutokea katika ukumbi wake.

Katika masumbwi hayo yasiyo rasmi, Mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema), Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ anadaiwa kumpiga kichwa Askari wa Bunge na kumchania sare na kung’oa kipaza sauti.

Monday 19 August 2013

Wafuasi wa Sheik Ponda wapiga kambi katika gereza la Segerea


Wafuasi wa Kiongozi wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Issa Ponda wamepiga kambi katika Gereza la Segerea, Dar es Salaam wakitaka kumwona bila mafanikio. 

Wakizungumza jana nje ya gereza hilo, wafuasi hao walisema walipofika hapo saa nne asubuhi waliambiwa kwamba tayari ndugu zake wanne walikwisharuhusiwa kuingia kumwona.


“Tumeambiwa kwamba idadi watu hao inatosha na kwamba wengine haturuhusiwi kumwona,” alisema mmoja wa wafuasi hao, Baraka Mohamed na kuongeza: “Tunaendelea kusubiri huruma za askari wa Magereza labda baadaye wanaweza kuturuhusu kumwona,” alisema.


Wafuasi hao ambao walijaza sehemu kubwa ya eneo la mapokezi na nje ya gereza hilo walilalamikia kitendo cha askari hao kutokuwaruhusu kumwona kiongozi wao.


“Nimefika hapa asubuhi na mapema, lakini utaratibu sikuupenda kwa kweli. Nimezuiwa nami nataka kumwona kiongozi wangu na si mimi tu tuko wengi hapa,” alisema mfuasi huyo.


Wafuasi hao hawakukata tamaa kwani licha ya kuzuiwa waliamua kukaa jirani na lango la gereza na wengine kusimama vikundi vikundi wakijadiliana namna ya kupata nafasi ya kumwona. Sheikh Ponda ambaye alikuwa amelazwa katika Taasisi ya Tiba na Mifupa Muhimbili (Moi) alipelekwa katika gereza hilo Alhamisi iliyopita.


Hatua hiyo ilikuja baada ya kusomewa shtaka la uchochezi akiwa kitandani akidaiwa kutenda kosa hilo katika maeneo mbalimbali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kati ya Juni 2 hadi Agosti 11 mwaka huu.


Kwa nini walizuiwa?

Ofisa Habari wa Jeshi la Magereza, Deodatus Kizinja alisema jana kuwa kisheria ni watu wawili katika kipindi cha wiki nne wanaoruhusiwa kumwona kila mahabusu.


Hata hivyo, alisema kwa kuzingatia sababu mbalimbali ambazo zimekuwa zikitolewa na wananchi, wamekuwa wakiruhusu idadi zaidi kila inapobidi.


“Kwa watu maarufu kama Ponda, Jeshi la Magereza linakuwa makini kudhibiti umati wa watu wanaotaka kumwona mahabusu kwa sababu hatuwezi kufahamu kama watu wote wana nia njema au la,” alisema Kizinja na kusisitiza kuwa ndugu zake wanne ambao walishaingia kumwona wanatosha.

Msemaji wa Familia ya Ponda, Isihaka Rashid alisema alikwenda katika gereza hilo kumwona kiongozi huyo Jumamosi iliyopita lakini alizungumza naye kwa muda mfupi akaomba akapumzike...  

“Jumamosi iliyopita tulimpelekea dawa, tukazungumza naye kwa muda mfupi akaomba akapumzike kwa sababu bado alikuwa anasikia maumivu,” alisema.

Lipumba ataka afutiwe mashtaka
Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba ameitaka Serikali imfutie kesi ya uchochezi Sheikh Ponda kwa madai kuwa ni ya kubambikiziwa.

Pia amelaani kitendo cha polisi kumwondoa Sheikh Ponda hospitali na kumpeleka gerezani huku akiwa bado anaendelea na matibabu ya jeraha alilopata.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Profesa Lipumba alisema: “Tunaitaka Serikali ifute makosa yote ya uchochezi aliyopewa Sheikh Ponda... kwani siku zote inafahamika mtu akisema ukweli anaonekana mchochezi.”


Waumini walia na Nchimbi, Shilogile
Wafuasi wa Sheikh huyo wamepanga kuandamana nchi nzima kushinikiza Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Morogoro, Faustine Shilogile waachie ngazi.

Wakizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika jana katika Viwanja vya Mwembe Yanga, Dar es Salaam walisema viongozi hao wameshindwa kuchukua hatua stahili kwa polisi waliohusika kumdhuru Sheikh Ponda.

Sheikh Ponda anadaiwa kupigwa risasi na polisi mjini Morogoro Agosti 10, mwaka huu.

Katika mkutano huo uliohudhuriwa na mamia ya wafuasi wake, viongozi wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania walieleza kutokufurahishwa na jinsi Jeshi la Polisi lilivyoshughulikia suala la Sheikh Ponda.

Mwakilishi wa Jumuiya hiyo, Sheikh Kondo Juma alisema Dk Nchimbi na Shilogile wanapaswa kuachia ngazi kutokana na kumbambikia kesi Sheikh Ponda.

Sheikh Juma alisema mbali na kutaka Shilogile ajiuzulu, alitaka kamanda huyo afikishwe mahakamani kutokana na Sheikh Ponda kujeruhiwa.

“Hawa viongozi wawili wanapaswa kuwajibika. Tutaandaa maandamano nchi nzima ili kushinikiza wajiuzulu,” alisema Sheikh Juma kwenye mkutano huo ambao pia ulihudhuriwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke, Englebert Kiondo.
Sheikh Juma alieleza kuwa ikiwa viongozi hao wataendelea kushikilia nafasi hizo, watakinyima kura CCM mwaka 2015.

CCM waombe radhi
Akizungumza katika mkutano huo, Kiongozi wa Kiislamu kutoka Zanzibar, Sheikh Salum Amour aliitaka Serikali ya CCM kuomba radhi kutokana na suala la Sheikh Ponda kuhusishwa na matukio ya umwagaji wa tindikali.
 
Pia alitishia kuwa isipoomba radhi, watainyima kura CCM kwenye uchaguzi ujao.

-Mwananchi.

Madiwani waliotimuliwa CCM wadai kuwa wako tayari kuhamia CHADEMA


MADIWANI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), waliofukuzwa katika Manispaa ya Bukoba, wamesema wako tayari kuhamia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kama chama chao kitaendelea na msimamo wa kuwafukuza. 


Akizungumza na MTANZANIA kwa njia ya simu jana, mmoja wa madiwani hao ambaye alikataa kutaja jina na kata yake, alisema wako tayari kuhamia Chadema muda wowote kama hawatarudishiwa uanachama wao.

Alisema, madiwani wote waliofukuzwa wana msimamo mmoja ambapo wanasubiri vikao vya Kamati Kuu ya CCM ili wajue hatima yao.

Kwa mujibu wa diwani huyo, wanachokifanya wao ni kutetea maslahi ya taifa na wananchi waliowapigia kura, wala siyo kulinda biashara za watu hata kama wanaungwa mkono na uongozi wa CCM.

Msimamo wa madiwani hao, umekuja siku mbili baada ya Mwenyekiti wa Taifa wa Chadema, Freeman Mbowe, kuwakaribisha Chadema madiwani wote waliofukuzwa katika manispaa hiyo na kwamba kama wakijiunga na chama hicho, watafundishwa siasa za mageuzi.

Mbowe aliwakaribisha madiwani hao katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Uwanja wa Uhuru Mjini Bukoba juzi, katika mwendelezo wa mikutano ya chama hicho ya mabaraza ya wazi yanayojadili rasimu ya Katiba mpya.

Katika mazungumzo yake, Mbowe alikwenda mbali na kusema chama chake kiko tayari kushirikiana na kiongozi wa CCM anayepinga ufisadi kama anavyofanya Mbunge wa Bukoba Mjini, Khamis Kagasheki.

Alipoulizwa kama wamepata mawazo ya kujiunga na Chadema, baada ya kauli ya Mbowe, diwani huyo alisema wao walishakuwa na mawazo hayo, lakini kauli ya mwenyekiti huyo imewaweka huru zaidi.

“Si kama tumeamua sasa, mawazo ya kuhamia Chadema tulikuwa nayo baada ya uongozi wa mkoa kutangaza kutuvua uanachama, lakini kwa kauli ya Mbowe, kutukaribisha rasmi Chadema, ametujengea moyo zaidi.

“Tatizo letu na meya linafahamika kwamba, ni ufisadi wake tulioulalamikia tangu mwaka jana kwenye vikao vya baraza la madiwani, hatukusikilizwa badala yake tunaonekana wasaliti wa chama.

“CCM wanapaswa kujua kwamba, hoja za wapinzani zikiwa sahihi wananchi wanawaunga mkono, vivyo hivyo na sisi hatuwezi kubeza hoja zao kwa sababu tu ni wapinzani, tutaonekana watu wa ajabu.

“Kimsingi, tumefarijika na kauli ya Mbowe, baadhi yetu tulikuwapo katika mkutano wake jana (juzi) pale Uwanja wa Uhuru, ni suala la muda tu mtasikia Bukoba imezaliwa upya,” alisema diwani huyo.

Balozi Kagasheki ambaye pia ni Mbunge wa Bukoba Mjini (CCM), anatajwa kuwa na uhasama wa kisiasa na kada mwenzake, Anatory Amani ambaye awali wawili hao walikuwa na ushirika wa karibu.

Alipotakiwa kuzungumzia suala la kufukuzwa kwa madiwani hao, Kagasheki alisema yeye hakuwepo katika kikao cha Halmashauri Kuu ya Mkoa kilichowavua uanachama.

Kuhusu taarifa za kutoelewana na Amani, alisema kila mmoja amekuwa na mtazamo wake juu ya mvutano huo.

“Kila mtu ana maoni yake, siwezi kuzuia hisia na maoni ya watu wengine, kila mtu anaweza kutoa maoni atakavyo, ngoja watu waseme,” alisema Kagasheki.

Madiwani wanane waliofukuzwa wanatuhumiwa kushirikiana na wenzao wa upinzani kusaini hati maalumu na kuiwasilisha kwa mkurugenzi wa manispaa, wakimtaka aitishe kikao ili wapige kura ya kumng’oa madarakani Meya Amani.

Kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Kagera kilichokaa Agosti 3 mwaka huu, kiliwafukuza uanachama na uongozi madiwani hao akiwamo Mwenyekiti wake wa Wilaya ya Bukoba, Yusuph Ngaiza na Diwani wa Kata ya Kashai.

Wengine waliofukuzwa ni Diwani wa Kata ya Buhembe, Alexander Ngalinda, Samwel Ruhangisa (Kitendaguro), Dauda Kalumuna (Ijuganyondo), Deus Mutakyahwa (Nyanga), Robert Katunzi (Hamugembe), Richard Gasper (Miembeni) na Murungi Kichwabuta ambaye ni Diwani wa Viti Maalumu.


-Mtanzania

Mtoto apigwa na kulishwa Mavi na baba yake mzazi huko Mara


MWALIMU wa Shule ya Msingi Morotonga, wilayani Serengeti, Mkoa wa Mara, Karata Mugunda, anashikiliwa na Jeshi la Polisi wilayani hapa, kwa tuhuma za kumpiga na kumlisha kinyesi mtoto wake wa kumzaa mwenye umri wa miaka 10. 


Mwenyekiti Mtendaji wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu, Wilaya ya Serengeti, Samwel Mewama, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba mtoto huyo alilishwa kinyesi alichokuwa amejisaidia ndani ya nyumba yao.

Kwa mujibu wa Mewana, tukio hilo la kusikitisha lilitokea Agosti 14, mwaka huu saa 12 alfajiri.

“Chanzo cha tukio hili la kikatili ni mtoto huyo kujisaidia haja kubwa ndani ya nyumba, baada ya kuogopa kutoka nje usiku wa manane.

“Baada ya kujisaidia, baba yake ambaye ni mwalimu, alikasirika na kuamua kumwadhibu kwa kumchapa fimbo sehemu za makalio na kumsababishia majeraha ya kutisha.

“Pamoja na kumwadhibu kwa fimbo, alimlazimisha ale kinyesi chote alichojisaidia kisha akamlazimisha anywe maji kwa wingi,” alisema Mewana.

Akizungumzia jinsi alivyopata taarifa za tukio hilo, alisema ofisi yake ilipigiwa simu na mwalimu mmoja anayefundisha shule moja na mtuhumiwa.

Baada ya taarifa hiyo, alifuatilia ili kujua ukweli wake ndipo alipomkuta mwanafunzi huyo akiwa amejeruhiwa vibaya makalio yake.

“Kwa kweli nilimkuta ana hali mbaya, kwa hiyo nilichokifanya nilimchukua na kumpeleka Kituo cha Polisi Mugumu nikapewa PF 3 kwa ajili ya matibabu hospitalini,” alisema.

Aliongeza kwamba, baada ya polisi kupata taarifa hiyo na kushuhudia majeraha aliyokuwa nayo mwanafunzi huyo kupitia dawati lao la kijinsia, walikwenda kumkamata mwalimu huyo ili hatua zaidi ziweze kufuata.

Daktari wa Zamu katika Hospitali ya Nyerere DDH, Dk. Ohoka Joseph, alithibitisha kuwapo kwa tukio hilo.

Alisema mtoto huyo alijeruhiwa vibaya kwenye makalio yake na kwamba ameathirika kisaikolojia.

“Huyo mtoto ameathirika kisaikolojia, kwa hiyo, kuna haja akafanyiwe uchunguzi kutokana na athari za kipigo na tukio alilofanyiwa.

SHEIK PONDA AFIKISHWA MAHAKAMANI CHINI YA ULINZI MKALI

Katibu Mkuu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu nchini, Sheikh Issa Ponda muda huu amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya mkoa wa Morogoro. 

Sheikh Ponda amefikishwa mahakamani hapo chini ya ulinzi mkali akisindikizwa na msafara wa magari yaliyokuwa na polisi. 
 
Ponda amesafirishwa kutoka jijini Dar es Salaam mpaka mkoani Morogogro kwa usafiri wa helkopta iliyotua katika viwanja vya Gymkhana.

Saturday 17 August 2013

DAKTARI ALIYEMTIBU SHEIKH PONDA MOROGORO ATIWA MBARONI...... CHAMA CHA MADAKTARI CHAPINGA NA KUDAI HANA KOSA



Kiongozi wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Ponda Issa Ponda ambaye alikuwa amelazwa katika Taasisi ya Tiba na Mifupa (Moi), jana aliondolewa na kupelekwa katika Gereza la Segerea, Dar es Salaam. 



Kitendo hicho kimelaaniwa vikali na familia yake na wafuasi wake, ambao wamepanga kufanya maandamano makubwa leo  ...



Sheikh Ponda, ambaye alisomewa shtaka la uchochezi akiwa kitandani na Mwendesha Mashtaka wa Serikali, Tumaini Kweka ilidaiwa kuwa alitenda kosa hilo katika maeneo mbalimbali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kati ya Juni 2 mpaka Agosti 11, mwaka huu.
Alisomewa mashtaka hayo mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Kisutu, Hellen Liwa.



Jana, Polisi waliimarisha doria kwenye Hospitali ya Taifa Muhimbili kuanzia saa 1:30 asubuhi. Magari matatu ya Kikosi cha Kutuliza Ghasia(FFU) yaliyobeba askari wenye silaha yalionekana yakiranda katika maeneo mbalimbali ya hospitali hiyo.


Sheikh Ponda alitolewa wodini saa 4:20 asubuhi chini ya ulinzi mkali wa askari baadhi yao wakiwa wamebeba silaha.
Alionekana akiwa ameshikiliwa na polisi kutokana na kukosa nguvu ya kutembea.

Akiwa amevalia shati lenye rangi ya udongo, kikoi cheupe na kandambili, Sheikh Ponda alipakiwa kwenye gari ndogo aina ya Landcruiser nyeupe lililokuwa na vioo vya giza.



Baada ya kupakiwa, safari ya kuelekea Segerea ilianza saa 4:45. Gari lililombeba lilitanguliwa na gari la FFU lililokuwa na askari wenye silaha likifuatiwa na magari mengine mawili ya FFU yaliyokuwa na polisi wenye sare na magari mengine mawili ambayo yalikuwa na askari kanzu.
 
Wakili ashangaa, familia yaja juu
Akizungumza baada ya tukio hilo jana, Wakili wa Sheikh Ponda, Juma Nassoro alisema hakuwa na taarifa za kuondolewa hospitali kwa mteja wake na kueleza kushangazwa na kitendo hicho akisema mteja wake alikuwa mgonjwa akiwa anahisi maumivu makali ya kidonda tangu juzi.


“Nimepigiwa simu mchana huu na mmoja wa wanafamilia, nimeshangaa sana kwa sababu nakumbuka jana (juzi Jumatano) Sheikh alishindwa kufanyiwa mahojiano na polisi kutokana na kuhisi maumivu na kizunguzungu,” alisema Nassoro.

Msemaji wa familia, Isihaka Rashid alisema hawakuwa na taarifa ya Sheikh Ponda kupata ruhusa ya kutoka hospitali na kwamba wakati anaondolewa alikuwapo mkewe na kijana mmoja kwani muda huo wanafamilia wengine walikuwa kwenye kikao.


“Nilifika hospitali asubuhi, hatukupewa nakala yoyote ambayo inaonyesha Sheikh Ponda karuhusiwa. Lakini baada ya tukio tulipokwenda kuhoji tukaambiwa wamemruhusu tukapewa na karatasi ya kuthibitisha kuwa ameruhusiwa,” alisema Isihaka.


Sheikh Ponda alifikishwa hospitalini hapo Jumapili iliyopita, akiwa na jeraha ambalo linadaiwa kuwa ni la risasi aliyopigwa na polisi katika mkutano wa Kongamano Mjini Morogoro. Rashid alisema familia imepatwa hofu juu ya usalama wa maisha yake kwa kuwa hali yake bado haijatengamaa kwani alikuwa amevimba mkono.


“Wamemchukua katika hali inayotia shaka kwa sababu hata dawa zake hawakumchukulia, cheti cha ruhusa ya daktari pia kimeachwa, gharama zake za matibabu yake ni Sh1.1 milioni. Tumeambiwa tuchague kama tunataka kulipia au vipi, kwetu tunaona kama wamemteka,” alisema Rashid.


Alisema kutokana na hali hiyo familia imeamua kulirejesha suala la kufuatilia usalama wa maisha ya Ponda mikononi mwa viongozi wa Jumuiya anayoiongoza ili walishughulikie na kwamba tayari wamewajulisha kwamba watatoa tamko leo kwenye Msikiti wa Mtambani uliopo Kinondoni.

 
Daktari matatani
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Morogoro, Faustine Shilogile amesema watamhoji daktari aliyemtibu Sheikh Ponda Mjini Morogoro. Hata hivyo, Kamanda Shilogile hakutaka kutaja jina la daktari huyo akisema atakuwa anaingilia kazi ya Kamati ya Haki Jinai ambayo ndiyo inayochunguza suala hilo.


Jeraha la Sheikh Ponda limezua utata baada ya mwenyewe kusema kuwa limetokana na risasi aliyopigwa na askari wa jeshi hilo huku polisi wakikana.


Daktari huyo anaaminika kuwa ni miongoni mwa mashahidi muhimu kwani anafahamu chanzo cha kidonda cha Sheikh Ponda.


Inaaminika kuwa alitibiwa katika zahanati ya Al Jamih iliyoko Msamvu baada ya tukio hilo, Ijumaa iliyopita.


Hata hivyo, Makamu wa Mwenyekiti wa Chama cha Madaktari Tanzania (MAT), Rodrick Kabangira alipinga kitendo cha daktari kuhojiwa akisema Baraza la Madaktari Tanzania ndilo lilipaswa kumhoji.

“Tayari kuna utata wa jeraha lenyewe na ukweli ni kwamba ripoti ya huyo daktari ni muhimu kwa umma kwani ndiyo itathibitisha chanzo cha jeraha,” alisema.


Alisema hakuna kosa lolote kwa daktari huyo kumhudumia Sheikh Ponda isipokuwa kama atakuwa ameandika taarifa tofauti za jeraha hilo.


“Tatizo kubwa ni kwamba Serikali imekuwa ikiruhusu uchunguzi kwa tume ambazo hazitoi majibu halisi kwa wananchi. Ingetumika tume ya kimahakama au baraza ambalo lina mamlaka hata ya kumfutia usajili wake kama atakuwa amedanganya,” alisema.


Msajili wa Baraza la Madaktari Tanzania, Parot Luwena alisema madaktari hutakiwa kufanya kazi kwa misingi ya taaluma zao wala siyo kwa shinikizo, hivyo kama kuna masuala mengine ambayo polisi wanahitaji, wanapaswa kuzingatia sheria za nchi.


Polisi waonya waandamanaji
Polisi imesema kwamba itadhibiti maandamano yanayotarajiwa kufanyika leo kushinikiza kuachiwa kwa Sheikh Ponda.


Msemaji wa Polisi, Advera Senso alisema jana kuwa maandamano yoyote hayatavumiliwa na jeshi hilo.

“Tunapiga marufuku maandamano yoyote, watakaoyafanya wafahamu kuwa jeshi litayadhibiti,” alisema.

Ubao wa matangazo ya Makao Makuu ya Polisi limebandikwa tangazo la kuwataka polisi kuwa tayari kukabiliana na vurugu zozote zitakazotokea.


Tangazo hilo limesema hali ya usalama siyo nzuri na kwamba askari polisi wanatakiwa kujiandaa kukabiliana na vurugu.

-Mwananchi.

UNYAMA:MWANAMKE ABAKWA NA KUCHOMEKWA KISU SEHEMU ZA SIRI HUKO SHINYANGA



Mwanamke mmoja anayekadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 25 hadi 30 amekutwa amekufa katika makaburi ya Majengo soko la mjini Kahama mkoani Shinyanga huku mwili wake ukiwa ametobolewa macho na kuonesha kupigwa na kitu kizito usoni.

Mwanamke huyo ambaye hajatambulika jina lake na anakotoka alikuwa amevaa Blauzi nyeusi yenye madoa meupe, viatu vyenye urembo wa silva, mnene kiasi, mweusi na mwenye nywele ndefu.
Mwili wa Mwanamke huyo amegunguliwa leo majira ya saa sita Mchana baada ya watu waliokuwa wanachimba kaburi kuuona mwili huo pembeni ya eneo hilo na kutoa taarifa Polisi.
Kwa mujibu wa majirani wanaoishi eneo la makaburi hayo, tukio hilo linakisiwa kutokea usiku wa kuamkia jana huku baadhi ya kina mama wakisema kuwa walisikia sauti ya mwanamke akipiga mayowe katika eneo la mnadani.  
Naye mwenyekiti wa kitongoji cha Majengo  Kaskazini Noel Mseven amesema amepata taarifa kutoka kwa wananchi na baada ya kufika katika eneo hilo walibaini kuwa sehemu za siri za mwanamke huyo ziliingiziwa kitu chenye ncha kali.  
Jeshi la Polisi wilayani Kahama limethibitisha kutokea kwa tukio hilo huku Mrakibu msaidizi wa Polisi Aziz Mayunga akitoa wito kwa wananchi kufika katika chumba cha kuhifadhia maiti ili kuutambua mwili huo.
MATUKIO KATIKA PICHA
 
MWENYEKITI WA MTAA NOEL MSEVEN AKIUFUNUA MWILI ILI WATU WAUONE.

 
MSEVEN AKIENDELEA KUWAONYESHA WATU MWILI HUO.
  
SAMAHANI KWA PICHA HIZI JAMANI,TUNAFANYA HIVI ILI WATU WAMTAMBUE MAANA HADI SASA HAJAPATA NDUGU.

 
HILI NDILO ENEO LA MAKABULI ALIPOKUTWA MAMA HUYO.

JESHI LA POLISI LIKIWA LIMEFIKA ENEO HILO KUUCHUKUA MWILI HUO.
 
WANANCHI WAKISAIDIANA NA POLISI KUUBEBA MWILI HUO.

 
MWILI UKIPELEKWA KUPAKIWA KWENYE GARI

 
MWILI UKIPAKAKIWA KWENYE GARI YA POLISI

 
KATIKA ENEO LA TUKIO MWILI UKIPAKIWA KATIKA GARI TAYARI KWA SAFARI YA MOCHWARI.

 
HILI NDILO KABULI LILIKOKUWA LIKICHIMBWA NA WATU WALIOUONA MWILI HUO.

 
MWILI UKIPELWA HOSPITALI

KUTEKWA KWA PONDA NI HARAKATI ZA SERIKALI KUWAPENDELEA WAKRISTO"....UJUMBE WA VIPEPERUSHI VINAVYOSAMBAZWA KWA WAISLAMU



SAKATA la Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Ponda Issa Ponda, limeendelea kuwa gumzo katika maeneo mbalimbali, huku matamko makali yakitolewa dhidi ya Serikali.

Sakata hilo limeonekana kutikisa na kutawala vyombo vya habari, baada ya kiongozi huyo wa dini kudaiwa kupigwa risasi, kusomewa mashtaka kitandani na baadaye kupelekwa gerezani chini ya ulinzi mkali akitolewa katika Taasisi ya Tiba na Mifupa (MOI).

Suala hilo limeibua hisia nyingine baada ya masheikh jijini Dar es Salaam, kutoa tamko lenye mwelekeo wa kupinga udhalilishwaji wa kiongozi huyo na kuionya Serikali juu ya mwenendo huo.

Mbali na masheikh kutoa tamko jana, Jeshi la Polisi kwa upande wake nalo liliimarisha ulinzi katika Msikiti wa Kichangani, uliopo Magomeni na ule wa Mtambani uliopo Kinondoni, jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Msemaji wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Rajab Katimba, alisema kitendo hicho ni kibaya kwani kinapandikiza chuki baina ya Waislamu na Serikali.

Sheikh Katimba ambaye alikuwa ameongozana na masheikh kadhaa akiwamo Amiri wa Shura ya Maimamu, Sheikh Musa Kundecha, alitoa tamko hilo katika Msikiti wa Mtambani, Kinondoni jijini Dar es Salaam jana.

“Tunalaani kitendo alichofanyiwa Sheikh Ponda, tukio la kupigwa risasi na baadaye kudhalilishwa kwa kuondolewa hospitali wakati akipatiwa matibabu, ni jambo baya linakwenda kinyume na haki za binadamu.

“Tukio hili limeibua hisia kali kwa Waislamu, hivyo tunaitaka Serikali kuacha kuwatesa na kuwadhalilisha viongozi wa dini ya kiislamu, kwani kufanya hivyo ni kupandikiza chuki miongoni mwa Waislamu.

“Waislamu wamekuwa wakiamini kwamba, ufumbuzi wa suala la amani ya kweli na ya kudumu ya nchi ni kuweza kushughulikia madai ya msingi ya Waislamu dhidi ya Serikali ambayo ndio chanzo cha madai ya kupigwa risasi kwa Sheikh Ponda,” alisema Sheikh Katimba wakati akisoma tamko hilo lililosainiwa na Sheikh Juma Said Ally.

Waitisha mkutano wa dharura kesho

Kutokana na suala hilo, jumuiya hiyo imeitisha mkutano wa hadhara utakaofanyika kesho katika viwanja vya Nurul Yakin vilivyopo Wilaya Temeke, jijini Dar es Salaam ambapo tamko litatolewa juu ya mustakabali wa suala hilo.

Katika tamko hilo, Sheikh Katimba alisema kuwa hatua hiyo inaweza kuzidisha chuki baina ya Waislamu na vyombo vya dola kwa madai kuwa vimekuwa vikiwakandamiza Waislamu.

“Kitendo cha kumpiga risasi Sheikh Ponda na kisha kumchukua kutoka hospitali na kumpeleka gerezani kwa kukiuka taratibu ni kinyume cha haki za binadamu.

“Matibabu ni haki mojawapo kwa binadamu yeyote hata kama kuna wanaomtuhumu. Tuhuma si sababu ya kukiuka taratibu, kuvunja sheria na hata kumtisha unayemtuhumu, kwani njia hiyo haiwezi kutatua bali inazidisha ukubwa wa tatizo.

“Tunalaani kwa mara nyingine kitendo cha Polisi na Usalama wa Taifa kutenda vitendo vinavyoashiria uonevu kwa viongozi wa dini ya Kiislamu, pia tunaitaka Serikali kutenda uadilifu kwa raia wake hata pale inapoamini kuwa raia hao wana makosa.

Sheikh Basaleh aonya

Kwa upande wake mjumbe wa Taasisi ya Wanazuoni wa Kiislamu Tanzania, Sheikh Alli Basaleh alikemea vikali tukio la kupigwa kwa Sheikh Ponda na kusema kuwa jamii inapaswa kupinga vitendo vya watu kuteswa na kunyanyaswa vinavyofanywa na vyombo vya dola.

“Hii ni ishara ya huko tuendako kwa baadaye, nchi inaweza kuingia kwenye machafuko, ni wazi kabisa hata katika mataifa ambayo amani imevurugika hali ilianza kama hivi kama njia ya kupinga uonevu wa Serikali dhidi ya watu wake.

“Tuwe makini na hali hii hakuna taifa lolote linaloweza kuhubiri amani pasipo kuwa na umoja na masikilizano baina ya viongozi wa Serikali na watu wake,” alisema Sheikh Basaleh.

Polisi waranda misikitini

Hata hivyo wakati viongozi hao wakiendelea na mkutano na waandishi wa habari jana, Jeshi la Polisi liliimarisha ulinzi katika Msikiti wa Mtambani ambapo gari tatu zilikuwa zikiranda nje ya msikiti huo huku zikiwa na askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU).

MTANZANIA iliwashuhudia askari hao wakiwa katika gari aina ya Defender zenye namba za usajili PT 2118 na PT 2083, ambazo zilikuwa nje ya msikiti huo.

Hata hivyo wakati askari wakiwa wanaranda katika eneo hilo la Msikiti, baadhi ya makundi ya Waislamu walikuwa wakigawa vipeperushi vilivyokuwa vimeandaliwa na Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania ambavyo vilihoji. “Kwa nini Serikali ya CCM imempiga risasi Sheikh Ponda?”

Mbali na Msikiti wa Mtambani, askari pia walikuwa wametanda katika Msikiti wa Magomeni Kichangani, ambapo anatoka Mwenyekiti wa Baraza Kuu la Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Kundecha.

MTANZANIA ilifanikiwa kunasa kipeperushi kilichosomeka kwa maneno yafuatayo; “Kwa nini Serikali ya CCM imempiga risasi Sheikh Ponda, polisi waliotaka kumuua sasa wamemteka kutoka Muhimbili hadi Segerea akiwa bado mgonjwa.

“Hii imefanyika ili mfumo wa kuwakandamiza Waislamu na kuwapendelea Wakristo uweze kudumu na kuweza kupewa fedha na Serikali chini ya Mkataba (MoU),” ilisomeka sehemu ya kipeperushi hicho.

Alipopigwa mkoani Morogoro

Agosti 10, mwaka huu akiwa mkoani Morogoro, Sheikh Ponda, alidaiwa kupigwa na kitu kinachodaiwa kuwa ni risasi, ambapo Agosti 15, mwaka huu Jeshi la Polisi nchini liliripoti kushikiliwa kwa askari anayedaiwa kufyatua risasi hiyo.

Katika mahojiano aliyofanya na Gazeti la MTANZANIA Agosti 11, mwaka huu, Sheikh Ponda alisema polisi walidhamiria kumuua kwa makusudi ili wapoteze ushahidi. Huku akidai kuwa jeraha lake analodai limetokana na kupigwa risasi.

Sheikh Ponda alieleza kuwa alipigwa risasi na polisi wakati akiwa kwenye gari na wenzake. “ Nilimuona kwa macho yangu askari mmoja ambaye alikua amevaa sare akinilenga kwa mtutu wa bunduki,” alisema Ponda.

Monday 5 August 2013

OMMY DIMPOZ APIMA HIV NA KUSEMA "SINUNUI WALA KUUZA MECHI TENA"


Hii Ndio Post Yake kwenye Instagram Ya Star Wa Single Mpya 'Tupogo'Ommy Dimpoz Kuhusu Kupima HIV Na Kuamua Kuto Uza au Kununua Mechi Tena.
Kwenye Interview ya simu niliyo fanya nae leo, Ommy ameniambia hizi ndio sababu za yeye kupima H I V 
  1. Kujua Afya ili ujilinde na uwe mtu bora.
  2. Kukinga wengine baada ya kujua afya yako pia ni muhimu.

JAJI FRANCIS MUTUNGI ATEULIWA KUWA MSAJILI MPYA WA VYAMA VYA SIASA...TENDWA KWA HERI

huyu ndio msajili mpya wa vyama vya siasa....................

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Mheshimiwa Jaji Francis S.K. Mutungi kuwa Msajili wa Vyama vya Siasa.

Taarifa iliyotolewa Dar Es Salaam leo, Jumatatu, Agosti 5, 2013, na kutiwa saini na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue imesema kuwa uteuzi huo ulianza Ijumaa iliyopita Agosti 2, 2013.

Jaji Mutungi anachukua nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa Msajili wa Vyama vya Siasa, Mhe. John Tendwa ambaye amestaafu Utumishi wa Umma kwa mujibu wa sheria.

Kabla ya uteuzi huo, Jaji Mutungi alikuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dodoma.

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu, DAR ES SALAAM.

WANYARWANDA WAANZA KUREJEA MAKWAO BAADA YA RAIS KIKWETE KUWAPA SIKU 14 ZA KUONDOKA

story yote iko hapa


Mamia ya wahamiaji haramu kutoka nchini Rwanda wakiwa na ng’ombe zaidi 900 wameanza kuondoka nchini kurejea kwao kutokana na agizo la Rais Jakaya Kikwete kuwataka waondoke Tanzania kabla ya siku 14. 

Aidha, imeelezwa kuwa kumekuwapo ongezeko la askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) mkoani Kagera hasa wilayani Ngara hali inayozua hofu kwa baadhi ya wananchi, huku ikiongeza msukumo kwa wahamiaji haramu kuondoka.

Akiwa katika ziara mkoani Kagera, Rais Kikwete alitoa agizo la kuwataka wote waliokuwa wakiishi nchini kinyume cha sheria waondoke mapema jambo lililotakiwa kuanza kutekelezwa Julai 29 na kukamilika Agosti 10 mwaka huu.

Alisema kuwa wahamiaji haramu na wale wanaoendesha ama kuhusika na ujambazi, uhamiaji haramu na uingizaji haramu wa mifugo waamue kuchukua hatua mwafaka za kuondoka mapema kabla vyombo vya ulinzi na usalama kuanza operesheni maalumu ya kuwasaka.

Tayari idadi kubwa ya wafugaji wenye makundi ya ng’ombe imeanza kuondoka kuelekea eneo la mpakani la Rusumo kutoka ardhi ya Tanzania ikiwa ni utekelezaji wa agizo hilo la Rais Kikwete.

Akizungumza na Mwananchi Jumapili kwa njia ya simu, Mkuu wa Wilaya ya Ngara, Costantine Kanyasu alisema kwamba idadi kubwa ya wafugaji waliokuwa wakiishi kinyume cha sheria, imeitikia wito wa agizo la Rais na kuanza kuondoka kwa hiyari yao.

Hata hivyo, alisema kuwa pamoja na idadi kubwa ya wahamiaji kuanza kuondoka, bado wapo ambao hawajaondoka kutokana na kudai kuwa na vibali walivyovipata kutoka Ofisi ya Uhamiaji na kubainisha kwamba vibali hivyo vitakaguliwa kwa umakini wakati wa operesheni maalumu ili kujua uhalali wake.

“Jambo hili la wahamiaji haramu lilikuwa kero kubwa, siyo tu kwa Wilaya ya Ngara, bali mkoa mzima wa Kagera, lakini tunashukuru sasa wameanza kuondoka, wamebaki hao wenye vibali. Ni lazima vibali hivyo tutavikagua maana vipo vilivyotolewa kinamna,” alieleza Kanyasu.

Alionya kwamba jukumu la kuwaondoa kwa nguvu wahamiaji haramu pamoja na wafugaji linasubiri muda wa mwisho ili kuanza kutekelezwa kama Rais Kikwete alivyoagiza.

Hofu ya Wanajeshi kuongezeka

Akizungumzia suala la wanajeshi kudaiwa kuongezeka wilayani Ngara, Kanyasu alisema kwamba katika wilaya yake kuna kikosi cha dharura kinachokaa katika moja ya kambi za JWTZ kikikuwa na idadi kubwa ya askari lakini wananchi hawakuwa na taarifa nacho ila kutokana na sababu za kiusalama.

“Unajua kuna kelele za hapa na pale na haya majibizano yanayotokea baina ya Rwanda na Tanzania. Haya ni kama yamewastua watu na kudhani kuwa askari wetu wa Kikosi cha Dharura waliopo hapa Ngara wameletwa maalumu kutokana na tahadhari,” alisema na kufafanua kuwa askari hao wapo siku zote kwa ajili ya kulinda mipaka ya Tanzania.

Hata hivyo, mkuu huyo wa wilaya aliwataka wananchi kutulia na kutoa ushirikiano kwa jeshi hilo.

Rais Kikwete aliagiza operesheni hiyo ya kuwaondoa wahamiaji haramu ifanyike katika Mikoa ya Kigoma, Kagera na Geita kwa wakati mmoja ikisimamiwa na vyombo vya ulinzi na usalama yaani JWTZ, Polisi, Usalama wa Taifa na Uhamiaji akiwaonya wahalifu kuwa hapatakuwa na mahali pa kukimbilia wala kujificha.

ROBERT MUGABE NDANI YA IKULU YA ZIMBABWE KWA MARA YA SABA....



Baada ya kutangazwa kuwa mshindi wa kinyan’ganyiro cha Urais wa Zimbabwe, Rais Robert Mugabe (89), amefikisha mihula saba ndani ya Ikulu ya nchi hiyo. 

Mugabe juzi alishinda tena kiti cha urais. Matokeo rasmi yalionyesha kuwa aliibuka na ushindi wa asilimia 61 wa kura dhidi ya mpinzani wake, aliyekuwa Waziri Mkuu, Morgan Tsvangirai ambaye alipata asilimia 34.

Chama cha Zanu-PF kinachoongozwa na Mugabe na kile cha MDC cha Tsvangirai, viliunda Serikali ya Muungano mwaka 2008.

Juzi, Tume ya Uchaguzi Zimbabwe (ZEC), ilimtangaza Mugabe kuwa mshindi katika uchaguzi wa Rais uliofanyika Jumatano iliyopita.

Zanu-PF pia kilipata ushindi mkubwa katika uchaguzi wa wabunge baada ya kujinyakulia viti 137 kati ya 210.

Hata hivyo, inaelezwa kuwa hali inaweza kuwa tete hasa baada ya matokeo hayo ambayo yalipingwa na Tsvangirai na chama chake cha MDC. 

Tsvangirai alisema Chama cha MDC kitaisusia Serikali ya Mugabe na kupinga matokeo ya uchaguzi mahakamani. Wasimamizi wa uchaguzi kutoka Umoja wa Afrika wamesema uchaguzi huo ulikuwa huru na wa haki.

Aidha, Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC), ilimtaka Tsvangirai akubali matokeo ya uchaguzi.

Wasiwasi

Malalamiko yanayotolewa sasa na wapinzani kuhusu uchaguzi huo yanazidisha uwezekano wa kuibuka machafuko kama yaliyotokea 2008.

  
Mwaka huo, Tsvangirai aliongoza katika duru ya kwanza ya uchaguzi wa Rais na Zanu-PF kilipinga ushindi huo. Ghasia na machafuko vilitokea na kusababisha kuuawa kwa mamia ya wafuasi wa Tsvangirai.

Umwagaji damu uliotokana na uchaguzi huo ulimfanya Tsvangirai ajitoe kushiriki katika duru ya pili ya uchaguzi na hivyo kutoa mwanya kwa Mugabe kutangazwa kuwa mshindi wa duru hiyo kirahisi.

Hata hivyo, shinikizo la kimataifa lililofuata, lilimlazimu Mugabe kuunda Serikali ya umoja wa kitaifa kwa kuishirikisha MDC.

Tayari wananchi wa Zimbabwe katika Mji Mkuu wa Harare wanaamini kwamba wanapaswa kuheshimu matokeo ya uchaguzi na kujiepusha na kuibuka kwa machafuko.

-Mwananchi.

MSIMAMO WA RAIS KIKWETE KWA RAIS KAGAME WA RWANDA WAUNGWA MKONO KWA ASILIMIA 100 NA WASOMI HAPA NCHINI....



 WASOMI  na  baadhi  ya  wanasiasa  wazalendo nchini wameunga mkono msimamo wa Tanzania uliotolewa na Rais Jakaya Kikwete kuhusiana na chokochoko zinazoanzishwa na Rwanda na wamemtaka Rais wa nchi hiyo, Paul Kagame, kukaa meza ya mazungumzo na waasi wa nchi hiyo walioko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), kwani amani haiwezi kutafutwa kwa njia ya mtutu wa bunduki.

Akizungumza na MAJIRA  kwa njia ya simu jana Mhadhiri wa Chuo cha St. Agustino, katika kitivo cha sayansi ya siasa, Prof. Mwesiga Baregu, alisema ushauri alioutoa Rais Kikwete kwa Rais Kagame ni mzuri, hauwezi kuleta athari zozote tofauti na kutumia mtutu wa bunduki kukabili waasi.

"Mimi nikiwa kama mtaalam wa kutatua migogoro suala la mazungumzo ni njia moja ambayo huwa inatumika mara kwa mara na inasaidia kuleta amani," alisema na kuongeza;


"Kutumia mtutu wa bunduki haileti tija kwa mataifa yote mawawili, hivyo ni busara itumike njia ya mazungumzo."


Alitoa mwito kwa nchi jirani kushirikiana kutatua mgogoro uliopo kwa njia ya mazungumzo baina ya Rwanda na DRC.

Kwa upande wake Mkuu wa Kitivo cha Elimu Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dkt. Kitila Mkumbo, alisema anakubaliana na kauli ya Rais Kikwete na anashangazwa na Rais Kagame ni kwa nini anachukizwa kuambiwa azungumze na waasi.

"Maana yake inaonekana hataki kushauriwa...ushauri huo ni kitu kizuri kinaweza kuleta maelewano," alisema Dkt. Mkumbo. Alisema Rais Kagame, anaonekana kama dikteta kutokana na kukataa kuambiwa ukweli na viongozi wenzake.

Alisema kauli ya Rais Kikwete, aliyoitoa kwenye hotuba yake ya mwisho wa mwezi wa saba hakugusia masuala ya vita na anaamini kwamba kwa karne hii sio mwafaka nchi kuingia kwenye vita kwani nchi zina matatizo mengi ambayo yanahitajika kupatiwa ufumbuzi.

"Alichoongea Rais Kikwete, ni msimamo unaotakiwa kuungwa mkono na Watanzania kwani yeye ndiye Amiri Jeshi Mkuu na hiyo ndiyo kauli ya nchi...hivyo alichosema ni sawa," alisema Dkt. Mkumbo.

Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri, Absalom Kibanda, alisema ameridhishwa na kauli ya Rais Kikwete, kwani ametumia lugha sahihi katika kueleza hali halisi, hivyo Watanzania wote wanatakiwa kumuunga mkono.

Alisema kwa hali ilivyo ni lazima Watanzania waungane katika masuala kama hayo ili kuleta mshikamano wa nchi.


Mwenyekiti wa Tanzania Labour Party (TLP) Augustino Mrema, alisema anamuunga mkono Rais Kikwete, kwa kauli yake hiyo.

Alisema Rais Kagame ameanza chokochoko dhidi ya Tanzania na kwamba hivyo, ndivyo alivyoanza hata Idd Amin. "Siungi mkono vita vitokee, lakini kama atatuchokoza basi tuwe wa mwisho kujibu mapigo," alisema Mrema.

 Aliyekuwa Mhadhiri UDSM, Dkt. Azaveri Lweitama, amezitaka nchi za Afrika Mashariki kukaa chini ili kuangalia jinsi ya kutatua mgogoro huo.

Alisema kuipiga Rwanda ni kazi ndogo sana, lakini hauwezi kumaliza tatizo kwa kutumia bunduki na badala yake ni vyema nchi hizo zikaangalia namna ya kumaliza mgogoro.

"Unajua mnaweza kuingia katika vita mkamuondoa Rias wa Rwanda, lakini bado mkatengeneza matatizo mengine kwa rais ajaye," alisema.

Alisema Kongo kuna waasi wa Rwanda na hata Rwanda pia kuna waasi wa kutoka Kongo, hivyo ni lazima kutafuta njia nzuri ya kutatua tatizo hilo.

Kwa upande mwingine, Dkt. Lweitama, alivitaka vyombo vya habari kutopotosha taarifa zinazozungumzia vita vikitokea hakuna mtu atakayebaki salama.

"Vyombo vya habari vijitahidi kuandika habari zisizo za uchochoezi, kwani hata ninyi pia ni Watanzania, naamini vita ikitokea hakuna mhariri wala mwandishi atakayebaki salama," alisema.

Alisema vyombo vya habari pia vina nafasi ya kukaa chini na kutafakari namna ya kumaliza mgogoro kwa kuwa vina nafasi kubwa kwa mustakabali wa taifa.

Uhusiano wa Tanzania na Rwanda unaelekea kupata mtikisiko baada ya Rais Kikwete kutoa ushauri kwa Serikali ya Rwanda kuzungumza na mahasimu wao.


 Rais Kikwete alitoa ushauri huo kwa nia njema kwa kuwa bado anaamini kuwa kama jambo linaweza kumalizwa kwa njia ya mazungumzo njia hiyo ni vyema itumike.

Ushauri ule aliutoa pia kwa Serikali ya Kongo na kwa Serikali ya Uganda. ambapo katika mkutano ule Rais Yoweri Museveni wa Uganda aliunga mkono kauli hiyo.

Tangu atoe ushauri huo viongozi wa Rwanga wamekuwa wakitoa kauli za kejeli dhidi ya Tanzania na Rais Jakaya Kikwete. Katika hotuba yake Rais Kikwete, alisema uhusiano wa Tanzania na Rwanda unapitia katika kipindi kigumu

-MAJIRA.

Saturday 3 August 2013

MREMBO SHINDANO LA MISS AFRICA AUAWA KWA KUCHOMWA VISU.


Mrembo chipukizi amekutwa amekufa kwa kuchomwa kwa visu huku binti yake wa miaka mitatu 'akilia pembeni yake kwenye dimbwi la damu', wamesema marafiki jana.

Mwili wa Linah Keza, mwenye miaka 29, ambaye inafahamika alishiriki kwenye Shindano la Miss Africa 2010, ulikutwa kwenye ghorofa moja huko King Edward Road, Leyton, juzi mapema asubuhi.
Tukio hilo liliripotiwa kwenye Tume Huru ya Polisi ya Malalamiko, ambayo itatazama mawasiliano yake waliyokuwanayo polisi na mwanaume mwenye miaka 38 ambaye amekamatwa kuhusiana na kifo chake.
Madaktari wa Huduma za Gari la Wagonjwa London waliongozana na polisi kwenda mahali hapo kabla ya Saa 10:30 alfajiri, lakini Linah, raia wa Rwanda anayeishi London, alikuwa ameshatangazwa kufariki eneo la tukio.
Inafahamika kwamba binti yake alikuwa mahali hapo wakati wa shambulio hilo, kwa mujibu wa fafiki mmoja wa familia hiyo.
Herbert Muhire alisema: "Binti (yake) amepelekwa kwenye uangalizi na kupatiwa tiba ya kisaikolojia na matukio mengine baada ya kukutwa akilia kando ya mama yake huyo aliyekuwa amelala kwenye dimbwi la damu.
"Familia na marafiki wameelezewa jinsi alivyokuwa ameuawa na kufa kifo cha kutisha.
Rambirambi kwa Linah kutoka kwa marafiki na jamaa ziliachwa kwenye ukurasa wa Facebook uliofunguliwa mara baada ya kifo chake.
Azun Jezan aliandika: "Huzuni mno, roho yake ilale mahali pema peponi na binti yake na familia wajazwe nguvu katika wakati huu mgumu wa huzuni."
Mwingine, Justine Twongyeirwe, aliandika: "Nitakumbuka tabasamu lako mpenzi Linah. Ulale Mahali Pema."
Jana asubuhi, ukurasa huo ulikuwa na wafuasi zaidi ya 500 na baadhi walituma picha za Linah, ambaye alifanya kazi kama mrembo na kusomea huduma za jamii kwenye Chuo Kikuu cha Wolverhampton.
Kwa mujibu wa polisi, mwanaume huyo mwenye miaka 38 alikamatwa baada ya kujisalimisha mwenyewe kwenye kituo cha polisi cha north London juzi.
Msemaji wa polisi alisema: "Uchunguzi wa mauaji umeanza baada ya mwanamke huyo kushambuliwa huko Leyton.
"Polisi waliitwa na Huduma za Gari la Wagonjwa London majira ya Saa 10:29 alfajiri ya Jumatano kwa ripoti za kuchomwa kwa visu.
"Maofisa na Huduma za Gari la Wagonjwa walifika na mwanamke huyo mwenye miaka 29 alikuwa ametangazwa kufariki kwenye eneo la tukio."
Uchunguzi wa mwili wake ulipangwa kufanyika majira ya Saa 5 jana asubuhi kwenye Mochari ya Walthamstow.