SIASA

TUTAIFUTA CHADEMA ENDAPO ITABAINIKA KUWA WALIRUSHA BOMU LA ARUSHA WENYEWE"....TENDWA

Msajili wa Vyama vya Siasa nchini John Tendwa,  amedai kuwa ikibainika kuwa CHADEMA ndio waliohusika katika kulipua bomu katika mkutano wao wa 15/06/2013 atakifuta.
Tendwa  ameyasema   hayo alipokuwa akizungumza katika kipindi cha Hot Mix cha East Africa Television akijibu swali la mtangazaji wa kipindi Adrian Stepp  kuhusu  hatua  zitakazochukuliwa...

Alipoulizwa kama itathibitika kuwa CCM ndio walihusika kulipua bomu hilo amedai kuwa hawezi kukifuta kwakuwa kwa kufanya hivyo itakuwa ni kufanya mapinduzi ya kalamu.




TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI: KUHUSU MAANDAMANO YA AMANI YA CHAMA CHA WANANCHI CUF.


THE CIVIC UNITED FRONT(CUF- Chama Cha Wananchi) 
TAREHE 29 JUNI 2013.
Waheshimiwa waandishi wa habari, kwa niaba yangu binafsi na kwa niaba ya uongozi wote wa kitaifa wa Chama chetu, naomba kuchukua fursa hii kuwakaribisha Ofisi Kuu ya chama ili tupate fursa ya kuzungumza nanyi na kwa maana hiyo kuzungumza na watanzania kupia kwenu ili ujumbe uliokusudiwa na chama uweze kuwafikia wananchi popote pale walipo.
Tumewaita leo tarehe 22 Juni 2013 tukiwa na agenda moja kuu nayo ni kuwaeleza kwamba Chama cha Wananchi CUF kimeandaa Maandamano ya Amani siku ya tarehe 29 Juni 2013 maandamano ambayo yataanzia eneo la Buguruni kituo cha Mafuta saa nne kamili asubuhi, kupitia barabara ya Uhuru, Mnazimmoja, Bibi Titi, Posta mpya , Aridhi hadi Ikulu.
Maandamano hayo ambayo yataongozwa na Mwenyekiti wa Chama taifa Profesa Ibrahim Haruna Lipumba, yanatarajiwa kupokelewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania au mwakilishi wake, na kwamba yanalengo la kufikisha malalamiko ya wananchi kutokana na vitendo vya ukatili vinavyofanywa na jeshi la polisi na jeshi la wananchi ambalo kimsingi taifa letu linaelekea mahali pabaya.
Waheshimiwa waandishi wabari, mtakumbuka tarehe 15 Juni 2013 wakati Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema wakihitimisha mkutano wa kampeni ya uchaguzi mdogo wa udiwani katika Kata nne za Arusha, palitokea mlipuko wa bomu uliopoteza maisha ya wananchi wane kwa mujibu wa taarifa za polisi na wengine wengi kujeruiwa vibaya.
Kwa kuwa jambo hili lipo katika hatua za uchunguzi, Chama cha CUF hakikusudii kuingilia uchunguzi unaoendelea lakini tunataka kufikisha ujumbe kwa rais kwamba hii si mara ya kwanza kuundwa kwa tume mbalimbali za uchunguzi hapa nchini. Kinachotusikitisha ni kuwa hata mara baada ya uchunguzi huo, hakuna ripoti inayotolewa hadharani kuonyesha chanzo cha tukio, wahusika na hatua zilizo au zinazotarajiwa kuchukuiliwa.
Tutamtaka Mheshimiwa rais kuhakikisha ripoti ya uchunguzi itokanayo na maafa yaliyotokea Arusha iwekwe wazi na serikali iwachukulie hatua stahiki wale wote watakaobainika kuhusika na tukio hilo ili iwe funzo kwa wengine au wale wenye kuwa na malengo yanayofanana na hayo kwa kuwa Tanzania ni yetu sote na haitowezekana watu wachache wayachezee maisha ya watu kwa sababu ya kukidhi matakwa binafsi ambayo hayana tija kwa jamii.
Maandamano pia yanalenga kuishinikiza serikali kukomesha vitendo vya kinyama, vitendo vya kijangili vinavyofanywa na Jeshi la Polisi na Jeshi la Wananchi wa Tanzania kwa kuwakamata, kuwatesa, na kubaka wananchi wasio na hatia wa Mkoa wa Mtwara na hasa wanaoishi katika wilaya za Mtwara Mjini, MtwaraVijijini, na Newala huku baadhi yao wakichomewa nyumba zao moto na wengine wakiporwa mali zao. 
Waheshimiwa waandishi wa habari, mtakumbuka hivi karibuni pamekuwa na fukuto la suala la gesi katika Mkoa wa Mtwara ambapo baadhi ya maafisa wa Serikali wamekuwa wakipotosha madai ya wananchi ikidaiwa kwamba wananchi wa mkoa huo wamesema hawako tayari kuona gesi yao inatumiwa na wananchi wengine kinyume na wale wa mikoa ya Lindi na Mtwara jambo ambalo si kweli lakini wanayafanya haya ili kuwajengea chuki dhidi ya watanzania wengine ionekane kwamba wananchi wa Mtwara na Lindi ni wabinafsi na wasioitakia mema nchi yetu.
Madai ya wananchi wa Mtwara yanatokana na uzoefu waliokuwa nao katika maeneo yote ambapo pana miradi ya kimaenedeleo itokanayo na maliasili ya nchi, maeneo hayo yamekuwa masikini na watu wachache wamekuwa wanatajirika, walichotaka kufahamu wananchi watanufaikaje na uwepo wa gesi katika maeneo yao kabla ya kuinufaisha nchi mzima kwa kuwa wao ndiyo watakuwa wa kwanza kuathirika ikiwa patatokea hitilafu yoyote itokanayo na uchimbwaji wa gesi hiyo.
Leo tunaweza kujifunza kutokana na uchimbaji wa Dhahabu Geita (GGM), uchimbaji wa Almasi Mwadui Shinyanga, Mgodi wa Dhahabu wa North Mara, Nyamongo na maeneo mengine mengi, nini hali ya maisha ya wananchi wa maeneo hayo.
Pamoja na upotoshwaji wa makusudi uliofanywa na unaoendelea kufanywa na watendaji wa serikali juu ya suala la gesi ya Mtwara, inashangaza hata Jeshi la Wananchi wa Tanzania ambalo lilionekana awali kutenda haki kwa wananchi wa Mtwara baada ya wananchi kukosa imani dhidi ya Polisi kutokana na wizi na uporaji wa mali za wananchi huku wakichoma moto baadhi ya maduka kwa lengo la kuhalalisha vitendo vya hujuma pamoja na kuchoma moto soko la Nkana Read, Jeshi lililojijengea heshima kwa jamii nalo limeanza kuingia mkumbo wa kuwatesa raia bila makosa.
Mwanzoni mwa wiki hii Mkurugenzi wetu wa siasa wa wilaya ya Mtwara Mjini Mhe. Saibogi ambaye pia ni mwenyekiti wetu wa serikali ya Mtaa alitekwa na wanajeshi na kumpeleka katika Kambi yao iliyopo barabara ya kwenda Nanyamba ambapo walimvua nguo na kumpiga mijeredi usiku kucha bila hatia na kumuachia asubuhi yake huku wakiahidi kuwakamata viongozi wengine wa CUF ili kutoa funzo kwa wale wanaopigania haki za wananchi.
Matukio ya namna hii si ya kuyafumbia macho na yanatengeneza serikali yenye kiburi isiyotokana na maamuzi ya raia. Maisha ya namna hii hayawezi kuendeshwa katika nchi inayojiita huru kama yakwetu na badala yake mambo haya yanatukumbusha enzi za utawala wa kikoloni ambpo CUF kamwe hatupo tayari kuruhusu vitendo vya kishenzi kuona vinafanyika nchini petu.
Tulikianzisha Chama hiki kwa madhumuni ya kuwaunganisha watanzania wote popote walipo, bila kujali itikadi zao, waweze kukataa aina yoyote ya uonevu, ukandamizaji, unyanyasaji, ubaguzi na udhalilishaji wa kisiasa au kiuchumi.
Aidha tuna dhamira ya kulinda, kutekeleza na kuzienzi haki za Binadamu pamoja na kuinua uchumi wa nchi kwa siasa zitumikie uchumi badala ya uchumi kutumikia siasa kama inavyofanyika hivi sasa. CUF tunaamini katika siasa za ustaharabu ambazo zitatuwezesha kuwa na jamii salama yenye mshikamano na ushirikiano katika kuijenga nchi yetu, lakini wenzetu wanatumia upole wetu na ustaharabu wetu kutufanyia vitendo vinavyokiuka utu wa mtu na hatimaye kila aliyepewa mamlaka ya kuongoza sehemu ya nchi yetu anageuka kuwa mfalme na kuamrisha kamata Yule, mpe kesi Yule na mwache Yule. Uvumilivu wetu usiwe mtaji kwa CCM na serikali yake kutufanya watakalo, nasi ni binadamu.
Waheshimiwa waandishi wa habari, maandamano yetu yanalenga pia kuitaka serikali kuwasikiliza wananchi wa Mtwara kwa kukaa nao chini, kujua hoja zao na kutoa ufafanuzi pale patakapobidi, sisi tunaamini wanazo hoja za msingi na wakisikilizwa serikali itaona namna ya kuzifanyia kazi hoja hizo badala ya kukurupuka na kutoa kauli za kibabe eti hawa wanachochewa na vyama vya siasa au pana watu wasioitakia mema nchi ndiyo wanachochea, kauli hizi zinajenga chuki na zanakosa uzalendo wa taifa. Haiwezekani hao wanaojiita ndiyo wazalendo halisi wawe wanaifidi nchi alafu tuendelee kukaa kimya kama vile wananchi wa kusini ni watu wasioweza kufikiri na kupambanua baya na zuri.
Wakati wananchi hawa walipopeleka maombi yao kupitia kwa Mhe. Mohamedi Habibu Mnyaa Mbunge wa Mkanyageni, ilikuwa nafasi nzuri kwa serikali kuweza kusikiliza maombi yao na kutoa maamuzi, badala yake siasa zikatumika, maombi yakakataliwa leo Bunge linaunda kamati ya uchunguzi iende mtwara wakachunguze nini ikiwa tayari hoja zao zilikataliwa?
Ieleweke kuwa nchi yetu itajengwa na watanzania wenyewe kwa kushirikiana na kusikilizana. Amani ya kweli itapatikana ikiwa haki itaonekana kutendeka kwa jamii yote. Waheshimiwa waandishi wa habari, haya ni sehemu tu ya mambo ambayo tunakusidia kumfikishia rais wetu ili aweze kuyafanyia kazi.
Mungu Ibariki CUF, Mungu ibarika Tanzania.

SERIKALI YA MAPINDUZI ZANZIBAR YATOA SALAMU ZA RAMBIRAMBI KWA MKUU WA MKA WA ARUSHA




Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imetuma salamu za rambi mbali kwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mh. Magesa Muhongo kutokana na vifo vya wananchi watatu wa Mkoa huo vilivyotokea kufuatia mripuko wa bomu uliotokea juzi katika viwanja vya Soweto Jijini Arusha.



Watu wasiopungua 70 waliripotiwa kujeruhiwa wakati wa mripuko huo kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni za uchaguzi katika Kata ya Soweto wa Chama cha Demokrasia ya Maendeleo { Chadema }.



Katika Taarifa ya rambi rambi ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar iliyotumwa kwa Mkuu huyo wa Mkoa wa Arusha na kutiwa saini na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alielezea kupokea kwa masikitiko na huzuni taarifa ya shambulio la kigaidi la bomu lililotokea tarehe 15 Juni mwaka 2013.



Balozi Seif alisema Taifa kwa mara nyengine tena limekumbwa na msiba wa njama za kigaidi zilizoua na kujeruhi rMkuu wa Koa wa Arusha aia wema wasio na hatia sambamba na tukio jengine linalofanana na hilo lililogharimu roho za wananchi wengine wakati wakiwa katika ibada Kanisani.

Balozi Seif alisema kwa niaba ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Wananchi na yeye binafsi anatuma salamu hizo za rambi rambi kutokana na maafa hayo na kuwaombea marehemu malazi pema na majeruhi wapone haraka ili waungane na wenzao katika ujenzi wa Taifa.

Halkadhalika Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar alisema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inaiunga mkono Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania katika jitihada zake za kupambana na ugaidi wa aina yoyote hapa Nchini.

Alieleza kwamba SMZ na Wananchi wa Zanzibar wako pamoja na wenzao katika kipindi hiki kigumu cha huzuni na maombolezo na kuwaomba wafiwa wawe na moyo wa ustahamilivu, uvumilivu na subra katika kipindi hichi.

Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania imeamua kutenga shilingi Milioni Mia Moja { 100,000,000/-} kama zawadi kwa kwa mtu ye yote atakayetoa Taarifa zitakazofanikisha kunaswa kwa mhalifu au watu wenye mtandao wa ulipuaji wa mabomu hapa Nchini.

DR. NCHIMBI AWAFARIJI WAHANGA WA BOMU NA KUTEMBELEA SEHEMU ILIYOLIPULIWA BOMU



Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Dk. Emmanuel Nchimbi akiwa katika viwanja vya Soweto Arusha palipotokea mlipuko wa bomu wakati wa kufunga kampeni za kuwania udiwani wa kata za jijini arusha za chama cha CHADEMA
??????????????????????
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Dk. Emmanuel Nchimbi akiwa katika viwanja vya Soweto Arusha palipotokea mlipuko wa bomu wakati wa kufunga kampeni za kuwania udiwani wa kata za jijini arusha za chama cha CHADEMA
??????????????????????
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Dk. Emmanuel Nchimbi akiwa katika viwanja vya Soweto Arusha palipotokea mlipuko wa bomu wakati wa kufunga kampeni za kuwania udiwani wa kata za jijini arusha za chama cha CHADEMA
??????????????????????
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Dk. Emmanuel Nchimbi akiwa katika viwanja vya Soweto Arusha palipotokea mlipuko wa bomu wakati wa kufunga kampeni za kuwania udiwani wa kata za jijini arusha za chama cha CHADEMA
??????????????????????
Askali wa JWTZ wakikagua gari la matangazo la chama cha chadema ambalo lilipigwa risasi kwenye tenki la mafuta lengo likiwa lilipuke, katika viwanja vya Soweto Arusha palipotokea mlipuko wa bomu na mashambulio ya risasi wakati wa kufunga kampeni za kuwania udiwani wa kata za jijini arusha za chama cha CHADEMA
??????????????????????
Askali wa JWTZ wakikagua gari la matangazo la chama cha chadema ambalo lilipigwa risasi kwenye tenki la mafuta lengo likiwa lilipuke, katika viwanja vya Soweto Arusha palipotokea mlipuko wa bomu na mashambulio ya risasi wakati wa kufunga kampeni za kuwania udiwani wa kata za jijini arusha za chama cha CHADEMA
??????????????????????
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Dk. Emmanuel Nchimbi ametembelea wahanga wa mlipuko na shambulio la risasi vilivyotokea katika viwanja vya Soweto Arusha wakati wa kufunga kampeni za kuwania udiwani wa kata za jijini arusha za chama cha CHADEMA
??????????????????????
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Dk. Emmanuel Nchimbi ametembelea waanga wa mlipuko na shambulio la risasi vilivyotokea katika viwanja vya Soweto Arusha wakati wa kufunga kampeni za kuwania udiwani wa kata za jijini arusha za chama cha CHADEMA
??????????????????????
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Dk. Emmanuel Nchimbi ametembelea wahanga wa mlipuko na shambulio la risasi vilivyotokea katika viwanja vya Soweto Arusha wakati wa kufunga kampeni za kuwania udiwani wa kata za jijini arusha za chama cha CHADEMA
??????????????????????
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Dk. Emmanuel Nchimbi ametembelea wahanga wa mlipuko na shambulio la risasi vilivyotokea katika viwanja vya Soweto Arusha wakati wa kufunga kampeni za kuwania udiwani wa kata za jijini arusha za chama cha CHADEMA
??????????????????????
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Dk. Emmanuel Nchimbi ametembelea wahanga wa mlipuko na shambulio la risasi vilivyotokea katika viwanja vya Soweto Arusha wakati wa kufunga kampeni za kuwania udiwani wa kata za jijini arusha za chama cha CHADEMA
??????????????????????
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Dk. Emmanuel Nchimbi ametembelea wahanga wa mlipuko na shambulio la risasi vilivyotokea katika viwanja vya Soweto Arusha wakati wa kufunga kampeni za kuwania udiwani wa kata za jijini arusha za chama cha CHADEMA
??????????????????????
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Dk. Emmanuel Nchimbi ametembelea wahanga wa mlipuko na shambulio la risasi vilivyotokea katika viwanja vya Soweto Arusha wakati wa kufunga kampeni za kuwania udiwani wa kata za jijini arusha za chama cha CHADEMA
??????????????????????


WABUNGE WA CHADEMA WAGOMA KUINGIA BUNGENI KUFUATIA BOMU LA ARUSHA...IGP ATOA NAMBA YAKE KWA MTU YEYOTE MWENYE TAARIFA

Wakati Jeshi la Polisi nchini limesema limepata taarifa za mwonekano wa mtu aliyetupa bomu katika mkutano wa kampeni wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Arusha, Mwenyekiti wa chama hicho Freeman Mbowe amesema wabunge wake leo hawataingia bungeni.
 
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Mbowe alisema wabunge hao watawasili Arusha kwa ajili ya kuungana na wananchi pamoja na wanachama kwenye msiba huo.

Alisisitiza kwamba kuanzia leo mahema yatawekwa viwanja vya Soweto kwa ajili ya kuomboleza msiba huo na  mara polisi wakimaliza uchunguzi wao na kutoa majibu juu ya vifo hivyo, marehemu hao watasafirishwa.

Wakati Mbowe anatoa kauli hiyo Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk Emmanuel Nchimbi akizungumza jana mjini Arusha na waandishi wa habari, alisema taarifa za awali zinaonesha mlipuko huo ni bomu la kutupwa kwa mkono (grumeti)  na hivi sasa timu ya wataalamu  ikiongozwa na Kamishna wa Operesheni Maalumu wa Jeshi la Polisi, Paul Chagonja inaendelea na uchunguzi wa tukio hilo.
 
Naye  Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini,  Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP), Said Mwema  katika taarifa yake kwa vyombo vya habari ameahidi kupambana na kuhakikisha wahusika wanapatikana.
 
Alitoa taarifa hiyo jana kwa waandishi wa habari Dar es Salaam na kusema hadi jana, watu waliothibitika kufa katika tukio hilo ni wawili na 68 ni majeruhi.
 
Waliokufa ni Katibu wa Baraza la Wanawake (Bawacha) wa Chadema, Kata ya Sokoni 1, Judith Moshi (25) na mtoto aliyejulikana kwa jina moja la Justin.
 
"Mpaka hivi sasa  watu waliokufa ni wawili  na wengine 68 wamejeruhiwa na mlipuko huo, lakini naahidi kuwa tutapambana na kuhakikisha tunawapata wahusika," alisema Mwema.
 
Sanjari na kupatikana taarifa juu ya mtu aliyetupa bomu, Mwema alisema  timu ya jeshi hilo imetumwa kutoka makao makuu kwenda Arusha kuongeza nguvu katika upelelezi.

Hata hivyo, hakufafanua zaidi juu ya mtuhumiwa huyo kutokana na kile alichosema taarifa husika  zinafanyiwa uchunguzi  kabla ya  kuwakamata watu sahihi waliohusika na tukio hilo.

Kwa mujibu wa IGP Mwema, timu ya polisi kutoka Makao Makuu inayoongozwa na makamishna wawili, imeondoka  kwenda mkoani Arusha kuongeza nguvu katika operesheni na upelelezi.
 
Timu hiyo inaongozwa na Kamishna wa Operesheni na Mafunzo, Paul Chagonja na Isaya Mngulu kutoka Idara ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai, wakishirikiana na vyombo vingine vya ulinzi.
 
Alisema polisi inafanya operesheni kali nchini kote kuhakikisha inawatia mbaroni watu wote waliowezesha, waliofadhili na waliotenda uhalifu huo.
 
"Kikubwa wananchi waendelee kuwa watulivu na waendelee kutoa ushirikiano kwa wakati wote uchunguzi ukiendelea," alisema.

IGP ametaka mtu yeyote atakayekuwa na taarifa za wahalifu hao, atoe taarifa kupitia namba yake ya simu ambayo ni 0754 785557 au kwenye kituo chochote cha polisi ili wakamatwe.
 
‘Kwa nini  iwe Arusha’ hii ni kauli ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mulongo aliyoitoa baada ya kutembelea majeruhi katika Hospitali za Mount Meru, St Elizabeth pamoja na Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Centre jijini.

“Nawapa pole sana ndugu zangu wa Chadema, na wana Arusha kwa ujumla pamoja na watanzania. Lakini najiuliza kwa nini Arusha …tukio hili limenihuzunisha sana na nawaomba tusiingize masuala ya kisiasa, tuache polisi wachunguze tukio hili kwani timu ya wataalamu kutoka Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ) pamoja na wataalamu wengine wanachunguza tukio hili na wahusika watachukuliwa hatua.’’
 
Mulongo ambaye tukio hilo la juzi limekuja ikiwa ni  mwezi mmoja tangu kutokea kwa mlipuko katika Kanisa Katoliki la Joseph Mfanyakazi la Olasiti, alisema jana anayefanya ulipuaji wa mabomu na kumwaga damu za watu mbalimbali na wengine kufa, ipo siku Mungu atamhukumu.
 
Kati ya majeruhi  59  waliolazwa kwenye hospitali hizo, wawili wamehamishiwa Hospitali ya KCMC kutoka Hospitali ya  AICC kwa matibabu. Wagonjwa wengi wamelazwa hospitali ya Selian ambao ni 40. Hata hivyo, wanane waliruhusiwa baada ya matibabu.
 
Mkuu wa Mkoa alisema  anajisikia mnyonge kutokana na matukio hayo mawili tofauti; mlipuko wa kanisani na la juzi wakati Chadema ilipokuwa ikihitimisha kampeni zake za udiwani kwenye kata nne za Themi, Kaloleni, Elerai na Kimandolu ambao hata hivyo uliahirishwa kutokana na tukio hilo.

Mulongo alitaka wananchi  wasihusishe na masuala ya kisiasa badala yake wawaachie polisi kuchunguza tukio hilo. Kwa mujibu wa Mulongo, watu kadhaa wamekamatwa.

Katika kipindi kisichozidi miezi miwili, mji wa Arusha umeshuhudia majeruhi wasiopungua 130, na vifo vya watu watano vilivyotokana na kurushwa mabomu na watu wasiojulikana katika mikusanyiko kanisani na kwenye mkutano huo wa siasa wa Chadema.

Katika tukio la mwezi uliopita katika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Joseph Mfanyakazi,  watu watatu walifariki na wengine wapatao 59 kujeruhiwa. 

Mmoja wa watuhumiwa ambaye ni dereva wa pikipiki maarufu kama bodaboda, Victor Ambrose  alifikishwa mahakamani akidaiwa kuhusika katika shambulio hilo.

Akizungumza na waandishi wa habari, daktari wa hospitali ya Selian, Paul Kisanga alisema walipokea wagonjwa 48  kabla ya wanane kuruhusiwa.
 
Alisema miongoni mwa wagonjwa hao, wamo watoto watano wanne wakiwa wa kiume na mmoja wa kike. Mtoto Fahad Jamal (7)  amelazwa kwenye wadi ya wagonjwa mahututi chini ya uangalizi wa madaktari.
 
Hospitali ya St Elizabeth wapo wagonjwa wanane na Mount Meru imepokea wagonjwa tisa. Mganga Mkuu wa Mkoa wa hospitali ya Mount Meru, Frida Mokiti alisema wamepokea miili ya marehemu wawili ambao ni Judith Moshi (25) ambaye ni Katibu wa Baraza la Wanawake (Bawacha)  kata ya Sokoni 1, Jijini Arusha pamoja na mtoto aliyejulikana kwa jina moja la Justin (13). 

Kwa mujibu wa majeruhi wa tukio hilo,  Abraham Samuel waliona kitu kikiwa kwenye mfuko wa rambo kikirushwa juu na baada ya muda mfupi walisikia vilio na wengine kuzimia.

Kitu hicho kilirushwa kabla ya  Mwenyekiti wa Taifa wa Chama hicho Taifa, Freeman Mbowe kuhitimisha kampeni za uchaguzi za udiwani wa kata nne za Jimbo la Arusha Mjini.
 
Mlipuko huo unadaiwa kuwa ulitokea jirani na gari la matangazo la Chadema, aina ya Mitsubishi Fuso lililokuwa karibu na jukwaa alilokuwa akitumia Mbowe.
 
Mwenyekiti wa Chadema, Mbowe amedai tukio hilo si la bahati mbaya bali lilipangwa na kundi la watu.
 
Akizungumza na waandishi wa habari jana, alisema wabunge wa chama hicho leo hawataingia bungeni bali watawasili jijini Arusha kwa ajili ya kuungana na wananchi pamoja na wanachama wa kwenye msiba huo.
 
Kwa mujibu wa Mbowe, marehemu Judith atapelekwa mkoani Kilimanjaro na Justin atapelekwa mkoani Tabora kwa ajili ya maziko mara baada ya polisi kukamilisha uchunguzi juu ya tukio hilo.
 
Alisisitiza kwamba kuanzia leo mahema yatawekwa viwanja vya Soweto kwa ajili ya kuomboleza msiba huo na  mara polisi wakimaliza uchunguzi wao na kutoa majibu juu ya vifo hivyo marehemu hao watasafirishwa.
 
‘’Nimetembelea majeruhi jana hospitalini lakini kwa Hospitali ya Selian, Arusha Lutheran Medical Centre majeruhi ni wengi lakini walioumia sana ni watoto kuna mtoto mmoja amekatika mkono na mguu ambaye ni Sharifa Jumanne na Amiri Ally ana vyuma vitatu mwilini mwake,’’ alisema Mbowe.
 
Ingawa polisi imesema inaendelea na uchunguzi wa tukio hilo kabla ya kutoa taarifa kamili, Mbowe aliwaambia waandishi wa habari kwamba zipo taarifa kwamba shambulio hilo liliambatana na risasi za moto.
Chama cha Wananchi (CUF) kupitia kwa Mwenyekiti wake, Profesa Ibrahim Lipumba, kimelaani tukio hilo na kutaka Serikali ichukue hatua za haraka na kukamata waliohusika na matukio hayo iwe fundisho.
 
“Hatuna sababu na tusijenge utamaduni wa nchi yetu kugeuka eneo ambalo palipo na mkusanyiko mabomu yanalipuka, Tanzania ni nchi ya amani, kwa matukio haya CUF tunalaani kwa nguvu zote na kutoa pole kwa familia zilizoathirika,” alisema Lipumba.

Lipumba alisema kitendo kilichofanyika katika mkutano huo wa Chadema ni unyama wa kutisha wenye makusudi ya kundi fulani kutekeleza azma yao dhidi ya chama, watu, kundi na viongozi.
 
Alisisitiza kuwa utamaduni huo wa kufanya unyama katika mkusanyiko wa watu  unapaswa kudhibitiwa mapema ili kuepusha madhara mengine ndani ya jamii kwa kusababisha vifo, ulemavu wa kudumu na familia tegemezi.
 
“Tumefikia hatua mbaya sana ya kufanya siasa za mabomu huu ni utamaduni unaopaswa kukemewa na kupingwa, matukio haya yanajirudia kutokana na Serikali  yenyewe kuyakaribisha kwa kushindwa kuwachukulia hatua kali wahusika, tunaomba dola ifanye ifanyalo katika uchunguzi wake na kuwakamata na kuwafikisha wahusika kwenye vyombo vya sheria,” alisisitiza.





KINANA AMBURUZA KORTINI MBUNGE MSIGWA BAADA YA KUMWUITA JANGILI


https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhv3HMOhW_At3jVE_cCAGe0KrQSQ_L5EI7LB5dWWEJCjv4hBApzh2Hiq-5-Z-xp2UTnYvAcz3yqyHU3sogjuzHwU_wf9I2-9Ir6cawWGU5j4-XhzAHNqPi8A4j01KyY_Ow46AIgWjnDZVx0/s640/CCM+DMV+298.JPG
KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Abdul-rahman Kinana amemfungulia kesi Mbunge wa Iringa Mjini, Peter Msigwa (Chadema), kutokana na kumtuhumu anajihusisha na ujangili na biashara haramu ya pembe za ndovu.
Kinana amefungua kesi hiyo katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kutokana na kitendo cha Mbunge huyo kutoa tuhuma hizo dhidi yake kwa nyakati tofauti nje na ndani ya Bunge, pia alikataa kuzikanusha na kumuomba radhi.
Inadaiwa kuwa Aprili 21 mwaka huu Msigwa ambaye ni Waziri Kivuli wa Maliasili na Utalii alitoa tuhuma hizo kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika Shule ya Msingi Mbuguni wilayani Nyamagana mkoani Mwanza.
Aidha alizitoa bungeni wakati akiwasilisha hotuba ya Kambi ya Upinzani katika Makadirio ya Bajeti ya Wizara ya Maliasili na Utalii mwaka 2013/2014. Katika hati ya madai, Kinana anadai kuwa kutokana na tuhuma hizo ameharibiwa tabia yake, uaminifu, hadhi yake kitaaluma na weledi na kumfanya achukiwe na kudharauliwa katika jamii.
Anadai jina lake na heshima ambayo ameijenga kwa muda mrefu, vimeharibiwa na Msigwa kwa nia mbaya, pia kwa tuhuma hizo anazosisitiza kuwa ni za uwongo, licha ya kumsababishia maumivu ya kisaikolojia, pia zimemsababishia hasara ya fedha.
Anadai kuwa kabla ya tuhuma hizo alikuwa katika hatua za mwisho za mchakato wa mazungumzo ya mradi wa ubia wa kilimo cha mboga na mwekezaji kutoka kampuni ya nje, lakini tuhuma hizo zimesababisha kampuni hiyo kuvunja majadiliano hayo.
Kinana anadai kuwa sababu iliyotolewa na kampuni hiyo kuvunja mazungumzo hayo ni kutajwa kwake na mbunge huyo kuwa ni jangili anayejishughulisha na biashara hiyo.
Kwa mujibu wa hati ya madai, Mradi huo ulikuwa na thamani ya Dola za Marekani milioni nne, Hisa za ushiriki wa Kinana zilikuwa ni asilimia 25 katika kipindi cha miaka mitano hivyo anatathmini kuwa amepata hasara ya Sh milioni 350.
Kinana anaiomba Mahakama hiyo imwamuru Msigwa amlipe fidia ya Sh milioni 350 kama hasara rasmi, pamoja na fidia ya maudhi na fidia ya hasara ikiwemo gharama za kesi.
Aidha anaiomba Mahakama imwamuru amlipe riba kwa kiwango kitakachopangwa na Mahakama, tangu tarehe ya hukumu hadi malipo ya mwisho, imwamuru kufuta tuhuma dhidi yake na kumuomba radhi kwa kuchapisha katika magazeti mawili ya Kingereza na mawili ya Kiswahili yanayosambazwa nchini.
Pia Mahakama itoe zuio la kudumu kumzuia Msigwa, au wakala wake kutoa au kuchapisha taarifa zozote za kashfa dhidi yake. Katika hati ya madai amenukuu baadhi ya kauli za Msigwa, ikiwemo "Kinana (naomba waandishi wa habari mnisikie na nyie Usalama wa Taifa mkapeleke habari) hana sifa za kupita barabarani na kuwaambia Watanzania waiamini CCM. Kinana mikono yake si misafi."
"Hata kwenye Nassaco, Shirika la Meli Tanzania kuna harufu ya ufisadi ndani yake; ajibu hoja...Kinana meli zake ndizo zinazohusika kubeba pembe za ndovu nchini. hajajibu hoja hizo! Kwa siku nchi hii tembo 67 wanauawa.
"Hao ndio wanaokifadhili Chama Cha Mapinduzi, halafu wanakuja eti kuwashawishi Watanzania muwasikilize na kwamba Chama Cha Mapinduzi eti ni kizuri."
".Haya mambo ninayoongea ni hatari kwa sababu haya yote ni majangili ni organized Crime. Ni mtandao wa Kimafia, uko duniani kote, unaweza ukatuua lakini wabunge tumesimama tunawatetea..."




RAIS JK KIKWETE ZIARANI ARUSHA


Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika Tonia Kandiero wakifurahia baada ya kuzindua barabara ya Minjingu-Babati-Singida nje kidogo ya mji wa Babati Mkoa wa Manyara. Anayeshuhudia kushoto ni Waziri wa Ujenzi Dkt John  Pombe Magufuli na kulia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwezeshaji) Dkt Mary Nagu


Mkurugenzi wa Benki ya Dunia kwa nchi za Tanzania, Uganda na Burundi Bw. Philippe Dongier akipanda mti kama kumbukumbu baada  ya  Rais Kikwete kuweka jiwe la msingi kwa ajili ya kuanza kwa ujenzi wa barabara ya Arusha Minjingu maene ya kijiji cha Mguu-wa-Zuberi wilayani Monduli, Mkoani Arusha.

Sehemu ya barabara ya Minjingu-Babati-Singida iliyozinduliwa na Rais Kikwete

Rais Kikwete akisalimiana na baadhi ya wanahabari wa mkoa wa Arusha baada ya kuweka jiwe la msingi kwa ajili ya kuanza kwa ujenzi wa barabara ya Arusha Minjingu maene ya kijiji cha Mguu-wa-Zuberi wilayani Monduli, Mkoani Arusha.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika Tonia Kandiero na viongozi wengine wakikata utepe  kuzindua barabara ya Minjingu-Babati-Singida nje kidogo ya mji wa Babati Mkoa wa Manyara. Anayeshuhudia kushoto ni Waziri wa Ujenzi Dkt John  Pombe Magufuli na kulia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwezeshaji) Dkt Mary Nagu

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Mbunge wa Viti Maalum (CHADEMA) Mhe Rose Kamili baada ya kuzindua mradi mkubwa  wa maji  wa Mwakonko Singida Mjini.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Waziri Mkuu Mstaafu Mhe Frederick Sumaye wakati wa mkutano wa hadhara mjini Katesh mkoani Manyara

Rais Kikwete akisalimiana na baadhi ya wananchi wa  mkoa wa Arusha baada ya kuweka jiwe la msingi kwa ajili ya kuanza kwa ujenzi wa barabara ya Arusha Minjingu maene ya kijiji cha Mguu-wa-Zuberi wilayani Monduli, Mkoani Arusha.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mkurugenzi wa Benki ya Dunia kwa nchi za Tanzania, Uganda na Burundi Bw. Philippe Dongier  wakielekea kuweka  jiwe la msingi kwa ajili ya kuanza kwa ujenzi wa barabara ya Arusha Minjingu maeneo ya kijiji cha Mguu-wa-Zuberi wilayani Monduli, Mkoani Arusha.

No comments:

Post a Comment